STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 1, 2014

Ebu angalia usajili kabla ya dirisha kufungwa usiku wa leo

http://static.goal.com/439600/439663.jpg
WAKATI dirisha la usajili kwa klabu barani Ulaya likifungwa usiku wa leo, chini ni baadhi ya wachezaji waliohama na kutua katika klabu zao mpya mpaka sasa tukielekea ukingoni.
  • Javier Hernendez 'Chicharito' ametua Real Madrid kwa mkopo akitokea Manchester United
  • Radamel Falcao ajiunga na Manchester United kwa mkopo wa msimu mzima
  • Arsenal inapigana kupata saini ya Matija Nastasic na Ron Vlaar
  • Lewis Holtby awasili Ujerumani Germany kwa mkopo wa kipindi chote cha msimu ambapo anajiunga na Hamburg
  • Tottenham inaongoza mbio za kumnasa Danny Welbeck ambapo Arsenal nao wanamtaka mshambuliaji huyo wa Manchester United
  • Mlinda mlango aliye na wakati mzuri katika klabu ya Chelsea Petr Cech anatakiwa na QPR
  • Arturo Vidal huenda akasalia Juventus baada ya Manchester United kushindwa mpango wa pauni milioni £30
  • Sandro anatgakiwa na QPR huku Tottenham wakihitaji pauni milioni £16
  • Victor Valdes yuko katika mazunguzmo ya kujiunga na Liverpool akiwa huru
  • Benjamin Stambouli amefanikiwa vipimo vya afya kabla ya kuelekea Tottenham
  • Neil Warnock anataka wachezaji wanne kujiunga na Crystal Palace 
  • Micah Richards beki wa Manchester City anaelekea kutua Fiorentina.
  •  Alvaro Morata ameondoka Real Madrid na kutua Juventus ya Italia kumpisha Chicharito
  • Dirisha la usajili linafungwa saa tano kamili usiku huu wa Jumatatu.

  • No comments:

    Post a Comment