STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 1, 2014

Messi aanza na gundu, yathibishwa yu majeruhi

http://www.barcapakistan.com/wp-content/uploads/2014/01/1388427761_extras_noticia_foton_7_3.jpgNYOTA wa klabu ya Barcelona, Lionel Messi huenda  akawa nje ya dimba kwa kipindi kifupi baada ya kudaiwa kuumia paja jana wakati wa Ligi Kuu ya Hispania.
Klabu ya Barcelona imetoa taarifa ikidai kuwa nyota wake huyo amepata majeraha ya paja katika mchezo waliopata ushindi mwembamba dhidi ya Villarreal jana. 
Katika taarifa iliyotumwa katika mtandao wa klabu hiyo, imedai Messi aliumia msuli wa nyuma ya paja katika mguu wake wa kulia lakini sio majeraha makubwa sana. 
Pia ilithibitisha kuwa mshambuliaji wao mwingine Munir El Haddadi naye aliumia nyama na vipimo vya wote wawili vinatarajiwa kufanyika leo kujua ukubwa wa matatizo ya nyota wake hao. 
Kuna hatari kubwa Messi akakosa mchezo wa kirafiki wa kimataifa kati ya Argentina na Ujerumani unaotarajiwa kuchezwa keshokuwa.

No comments:

Post a Comment