STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 1, 2014

Beki Manchester City Micah Richards atimkia Fiorentina

http://www.ljsfoundation.org.uk/wp-content/uploads/2013/12/Micah-Richards_4.jpg
Micah Richards
BEKI wa klabu ya Manchester City, Micah Richards anatarajiwa kujiunga na klabu ya Fiorentina ya Italia baada ya kumaliza miaka 12 akiwa Etihad. 
Richards, 26 tayari ameshawasili Italia na anatarajiwa kuwa Mwingereza wa 24 kuichezea klabu hiyo mara atakapokamilisha usajili wake. 
Beki huyo alikuwa mchezaji muhimu ya kikosi cha City kilichonyakuwa taji la Ligi Kuu mwaka 2012 lakini amejikuta akikosa nafasi ya kucheza chini ya meneja Manuel Pellegrini aliyeibebesha ubingwa msimu uliopita. 
City pia bado wanasiliza ofa kwa wachezaji wao Matija Nastastic, John Guidetti na Scott Sinclair ambao wanaonekana kutokuwepo katika mipango ya Pellegrini. 
Richards ambaye ni mzaliwa wa Birmigham alifanikiwa kucheza mechi mbili pekee za Ligi Kuu msimu uliopita na alikuwa amebakiza mwaka mmoja katika mkataba wake.

No comments:

Post a Comment