STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 11, 2014

Ruvu Shooting kupimana ubavu na 94 KJ Lugalo leo jioni

TIMU ya maafande wa Ruvu Shooting inayojiandaa na Ligi Kuu Tanzania Bara jioni ya leo inatarajiwa kushuka dimba la Lugalo kuvaana na maafande wenzao wa 94 KJ katika mchezo wa kirafiki.
Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa muda mfupi uliopita na Afisa Habari wa timu hiyo, pambano hilo ni maalum kwa ajili ya kumpa nafasi kocha wao Mkenya Tom Olaba kuangalia mapunfugu wa kikosi chake dakika za mwisho mwisho kabla ya kujichimbia kuisubiri Ligi itakayoanza Septemba 20.
Timu hiyo ambayo ilimaliza katika nafasi ya sita msimu uliopita ikilingana pointi na Simba na Kagera Sugar kila moja ikiwa na 38, inasema wanaamini timu hiyo ya 94 KJ iliyopo Ligi Daraja la Kwanza itawapa mazoezi ya kutosha vijana wao katika pambano hilo la leo.
Ruvu iliyoingia kambini tangu Juni 9 imekuwa ikichgeza mechi kadhaa za kirafiki tayari kwa ajili ya Ligi Kuu ambapo watafungua dimba kwa kuumana na maafande wa Magereza, Prisons Mbeya katika pambano litakalochezwa kwenye uwanja wa Mabatini.
Msimu uliopita walifungua dimba na wapinzani wao hao na kuwanyuka mabao 3-0, kitu ambacho Bwire anaamini hata msimu huu mambo yatakuwa hivi hivyo katika pambano hilo la ufunguzi wa ligi Jumamosi ijayo.

No comments:

Post a Comment