STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 11, 2014

Chicharito amvulia kofia Ronaldo, adai ni bora kuliko Messi

http://www.lapatilla.com/site/wp-content/uploads/2011/10/balon-de-oro-2011_323x216.jpg
MSHAMBULIAJI mpya wa Real Madrid, Javier Hernandez 'Chicharito' amesema tayari ameshawishika kwamba Cristiano Ronaldo ni bora zaidi ya Lionel Messi.
Mchezaji huyo wa kimataifa wa Mexico amejiunga na mabingwa hao wa Ulaya kwa mkopo wa msimu mmoja akitokea Manchester United muda mfupi kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.
Hata hivyo, Chicharito, ambaye alitua Old Trafford mwaka mmoja baada ya Ronaldo kutimkia Madrid, amesema tayari amedatishwa na mambo makubwa yanayofanywa na Mreno huyo mazoezini.
Bila ya shaka, Ronaldo ndiye bora," mshambuliaji huyo mwenye miaka 26 aliliambia gazeti la El Chiringuito.
"Katika muda mfupi niliokuwapo hapa, nimemuona yeye ndiye bora zaidi duniani.
"Si kwamba hufanya vyema sana katika mechi tu bali hata kila siku.
"Kwangu mimi, Cristiano ndiye bora zaidi. Messi yuko matawi hayo pia; baada ya Cristiano, anafuatia Muargentina yule."

No comments:

Post a Comment