STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, September 11, 2014

Mama Mkwe wa Jennifer Mgendi kutolewa Sept 22

FILAMU mpya ya muimbaji nyota wa Nyimbo za Injili nchini, Jennifer Mgendi iitwayo 'Mama Mkwe' itatolewa rasmi Septemba 22 mwaka huu.
Akizungumza na MICHARAZO, Mgendi alisema filamu hiyo iliyokamilika hivi karibuni akiwa ameigiza na wakali wa filamu na miondoko ya Injili akiwamo Mussa Banzi na Bahati Bukuku itatoka mtaani siku hiyo.
Mgendi amewataka mashabiki wa filamu wasiikose filamu hiyo kutokana na kubeba ujumbe mwanana wenye mafunzo makubwa kwa jamii.
Alisema filamu hiyo iliyoongozwa na Mgeni Khamis na Chrissant Mhega wa Mega  Video Production imekamilika wiki iliyopita.
Mgendi anayetamba na albamu ya Hongera Yesu, alisema ndani ya filamu hiyo inayozungumzia mkasa wa mama mkwe anayemlilia mwanae wa kiume kumletea mjukuu na kuzua kizaazawa wamo pia Senga,Bi Bi Esther, Christine Matai, Husna Chobis. yeye (Mgendi)  na wengine ambao wameinoigesha vilivyo.
"Nimekamilisha filamu yangu mpya ya 'Mama Mkwe' ambayo nimeigiza mimi, Bahati (Bukuku) Christine Matai, Senga, Bi Esther, Mussa Banzi na wengine. Ni filamu yenye mafunzo makubwa kwa jamii na hasa mama wakwe wanaoingilia ndoa za watoto wao," alisema.
Kabla ya filamu hiyo, Jennifer amewahi kutamba na filamu kadhaa kama 'Chai ya Moto', 'Joto la Roho', 'Teke la Mama', na 'Pigo la Faraja'.

No comments:

Post a Comment