STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, September 10, 2014

Vijana CUF wahimiza kuchangamkia uchaguzi mkuu

http://3.bp.blogspot.com/-Vg1FlLMzmC8/UGVoED0VOGI/AAAAAAAByBI/GI-uXRyYJ-s/s320/tz%7Dcuf.gif 
Na Suleiman Msuya 'Kipimo'
JUMUIYA ya Vijana ya Chama Cha Wananchi (JUVICUF) imewataka vijana wa chama hicho kujitokeza kugombea katika chaguzi za vijana pamoja na ule wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika hivi karibuni nchini kote.
Rai hiyo imetolewa na Naibu Katibu Mkuu wa (JUVICUF) Hamidu Bobali wakati akizungumza na mwandishi wa habari katika ofisi za chama cha CUF jijini Dar es Salaam.
Alisema chama kupitia (JUVICUF) kinatarajia kufanya chaguzi kuanzia matawi, kata, wilaya na Taifa ambapo wilaya 45 za Tanzania Bara na 10 za Zanzibar zitashiriki ili kupatikana kwa viongozi.
Bobali alisema mikakati (JUVICUF) ni kuhakikisha kuwa chama kinajijenga vizuri kuanzia ngazi za chini hasa ukizingatia kuwa ni wakati wa uchaguzi wa Serikali za Mitaa na uchaguzi mkuu.
“Napenda kutumia nafasi hii kuwahimiza vijana wa CUF kujitokeza katika chaguzi zote za chama katika ngazi ya vijana ambazo zimeanza kufanyika sasa na mwezi ujao Novemba ili mwezi Desemba tuweze kufanya uchaguzi mkuu wa vijana Taifa”, alisema.
Bobali alisema uchaguzi huo wa Taifa unatarajiwa kuhusisha zaidi ya vijana 135 kutoka Bara na 120 kutoka Zanzibar ambao watotokana na chaguzi katika ngazi za Wilaya.
Alisema mikakati yao ni kuhakikisha kuwa wanakuwa na wawakilishi kutoka Wilaya zote za Tanzania Bara kama ilivyo Zanzibar ambayo italeta ushindani wa kisiasa hapa nchini.
Naibu Katibu huyo alisema pia JUVICUF inajipanga kufanya operasheni mbalimbali ambazo zitakuwa na lengo la kuhamasisha vijana kujitokeza katika chaguzi na ufahamu juu ya lengo la Wabunge wanaounga mkono Rasimu ya Jaji Warioba kutoka nje ya Bunge.
Alisema kuna hali ya sintofahamu kwa baadhi ya vijana na wananchi mbalimbali ya nini sababu ya wajumbe wa UKAWA kutoka nje ya Bunge hivyo JUVICUF inaona ni wakati muafaka wa kutoa elimu.
Bobali alisema ni vema vijana wa vyama vinavyounga mkono UKAWA kuendelea kuwa na umoja ili kuhakikisha kuwa juhudi za viongozi wao wa Kitaifa zinafikiwa ili waweze kukomboa Taifa.

No comments:

Post a Comment