STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 12, 2014

HUYU NDIYE MISS TANZANIA WA 20

MISS Tanzania mpya Sitti Abass Zuberi Mtemvu akipunga mkono mara baada ya kuvikwa taji hilo usiku wa kuamkia leo katika shindano lililoshirikisha warembo 30 na kufanyika ukumbi wa Mlimani City Dar es Salaam. Sitti Mtemvu ametwaa taji hilo lililokuwa likishikiliwa na Happyness Watimanywa na kuwa mrembo wa 20 tangu shindano hilo liliporejeshwa tena nchini mnamo mwaka 1994 na kutwaliwa na Aina Maeda.

Mrembo wa Redd's Miss Tanzania 2014, Sitti Abbas Mtemvu akiwa katika picha ya pamoja na Mshindi wa pili, Lillian Kamazima (kulia) na Mshindi wa Tatu, Jihhan Dimachk mara baada ya kutawazwa rasmi usiku huu kwenye ukumbi wa Mlimani City,jijini Dar es Salaam. Sitti Mtemvu alianza kwa kunyakua Redds Miss Chang'ombe na baadaye Redds Miss Temeke. Sitti ni binti wa Mbunge wa Temeke, Mhe. Abbas Mtemvu.
Picha zote na Othman Michuzi.
Redd's Miss Tanzania aliemaliza muda wake,Happiness Watimanywa akimpisha crown,Redd's Miss Tanzania wa sasa,Sitti Mtemvu.

























No comments:

Post a Comment