STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, October 12, 2014

Ureno yafumuliwa na Ufaransa, Benzema zaidi ya Ronaldo

http://level3.soccerladuma.net/cms2/image_manager/uploads/News/179201/7/default.jpg
Benzema akifunga bao la kuongoza la Ufaransa
http://i.dailymail.co.uk/i/pix/2014/10/11/1413055734828_lc_galleryImage_Portugal_s_Cristiano_Rona.JPG
Ronaldo akilalamika
https://media.zenfs.com/en_GB/Sports/Eurosport/1330493-28603425-2560-1440.jpg
Wachezaji wa Ufaransa wakimpongeza Pogba baada ya kufunga bao la pili la nchi yake wakiilaza Ureno 2-1
TIMU ya taifa ya Ufaransa imeitambia Ureno kwa kuilaza mabao 2-1 katika pambano la kirafiki la kimataifa, huku ikishuhudiwa nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo akishindwa kumaliza pambano kwa kuumia goti.
Mwanasoka Bora huyo wa dunai alitoka uwanjani dakika ya 76 baada ya kuumia akiwa ameshuhudia mchezaji mwenzake ambaye hivi karibuni alimwagia sifa akidai ndiye namba 9 Bora duniani akiwa amefunga bao moja na Paul Pogba akifunga la pili.
Benzema anayecheza na Ronaldo katika klabu ya Real Madrid alifunga bao la kuongoza dakika ya tatu tu kabla ya Pogba anayecheza Juventus kuongeza la pili dakika ya 65 na Ureno ilipata la kufutia machozi dakika ya 78 lililofungwa na mtokea benchi Ricardo Quaresma kwa mkwaju wa penati.

No comments:

Post a Comment