
Uingereza ilikwenda mapumziko wakiwa mbele kwa mabao mawili kabla ya kluongeza mengine matano katika kipindi cha pili na kuwafanya kuibuka na ushindi mnono wa mabao 5-0 katika mchezo huo.
Hudgson amesema kikosi chake kifanya kazi ngumu kuipenya ngome ya San Marino iliyowapa usummbufu lakini utulivu na subira kwa wachezaji wake vilifanya mchezo huo kuja kuonekana rahisi.
Mabao ya Uingereza katika mchezo huo yalifungwa na beki Phil Jagielka, nahodha Wayne Rooney aliyefunga kwa penati, Danny Welbeck, Andros Townsend na bao la kujifunga wenyewe lililofungwa na Alessandro Della Valle aliyebabatizwa na mpira uliopigwa na Rooney.
Ushindi huo unawapeleka Uingereza kileleni mwa msimamo wa kundi E kwa tofauti ya mabao dhidi ya Lithuania baada ya timu zote hizo kushinda mechi zao mbili walizocheza.
No comments:
Post a Comment