STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 18, 2014

Chelsea wapewa Liverpool Kombe la Ligi, Spur v Sheffield Utd


http://i2.mirror.co.uk/incoming/article4591109.ece/alternates/s615/Liverpool-v-Chelsea.jpg
Kivumbi kitakuwa kwao Januari 20/27
http://www.capitalonecup.co.uk/cms_images/trophypitchside800x600304-589134_478x359.jpg
DROO ya Nusu Fainali ya michuano ya Kombe la Ligi maarufu kama Capital One, imetoka ikionyesha kuwa Chelsea watakutana uso kwa uso na Liverpoo ambayo usiku wa jana ilipata ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya timu ya AFC Bournemouth.
Vijogoo vya London ya Kaskazini, Tottenham Hotspur walioifumua Newcastle United kwa mabao 4-0 yenyewe imepangwa kumenyana na Sheffiled United katika hatua hiyo ya nusu fainali.
Chelsea walioilaza Derby Count mabao 3-1 wataanzia ugenini kwenye uwanja wa Anfield na kama mambo yataenda kwa sare watarudi nyumbani kuivutia pumzi wapinzani wake.
Kwa upande wa Spurs wenyew wataanza nyumbani kabla ya kumalizia ugenini na mechi za mkondo wa kwanza zitachezwa Januari 20, 2015 na zile za marudiano kujua timu mbili zitakazocheza fainali.

No comments:

Post a Comment