STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 18, 2014

Prof Tibaijuka agomaa kujiuzulu, adai hata JK atamshangaa akifanya hivyo

http://www.fullshangweblog.com/wp-content/uploads/2014/06/DSC_0019.jpg
Prof Tibaijuka
TOFAUTI na matarajio ya wengi kwamba huenda angefuata nyayo za Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Jaji Fredrick Werema aliyetangaza kubwaga manyanga kwa hiari yake, Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, Prof. Anna Tibaijuka amegoma kujiuzulu kwa kudai haoni sababu ya kufanya hivyo
Akziungumza mapema leo jijini Dar es Salaam, Waziri huyo alisema watu wanaona kujiuzulu ni 'fasheni' ila kwake hayupo kwenye mkumbo huo na wala hana mpango huo kabisa.
"Nikijiuzulu hata Rais atanishangaa maana katika yale mapendekezo ya Bunge hakuna sehemu iliyonitaka kujiuzulu" alisema Prof Tibaigana.
Prof Tibaijuka, alisema kilichomfanya akutane na waandishi wa habari ni kuzungumzia yale aliyokosa nafasi ya kutolea ufafanuzi juu ya tuhuma zinazomkabili katika sakata la uchotwaji wa fedha za Akaunti ya Tegeta Escrow.

No comments:

Post a Comment