STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 17, 2014

Ander Herrera akanusha kupanga matokeo

http://www4.pictures.zimbio.com/gi/Manchester+United+v+Valencia+ODBuEmnisftx.jpg
KIUNGO wa klabu ya Manchester United, Ander Herrera amesisitiza kuwa hajawahi kushiriki zoezi lolote la upangaji matokeo wakati akiitumikia timu ya Real Zaragoza.
Nyota huyo wa kimataifa wa Hispania ametajwa katika kundi la watu 41 wakiwamo  wachezaji, makocha na wakurugenzi katika uchunguzi wa kashfa ya upangaji matokeo katika Ligi Kuu nchini Hispania maarufu kama La Liga.
Herrera aliandika katika ukurasa wake wa mtandao wa kijamii wa facebook kuwa hajawahi na kamwe hatathubutu kujihusisha na suala la upangaji matokeo kwani anaupenda mchezo wa soka na anaamini katika mchezo wa haki ndani na nje ya uwanja.
Waendesha mashitaka katika kashfa hiyo wanadai kuwa fedha taslimu euro 965,000 zililipwa kwa kocha Javier Aguirre na wachezaji tisa wa Zaragoza, ikiwa ni pamoja na Herrera, kabla ya mchezo wa La Liga mwishoni mwa msimu wa 2010-2011.
Herrera aliondoka Zaragoza na kujiunga na timu ya nyumbani kwao ya Athletic Bilbao mwezi Agosti 2011, kabla ya kujiunga na United mwezi Juni 2014.
Wengine waliohuzsishwa na kadhia hiyo ni nahodha wa Atletico Madrid, Gabi na beki Montero na kocha wa zamani wa Zaragoza aliyepo Japan kwa sasa.

No comments:

Post a Comment