STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 17, 2014

Shamsa: Sikuwa naigiza, kipigo cha Simba kiliniliza Taifa

Shamsa Ford katika pozi
Shamsa akiangua kilio jukwaani wakati Yanga wakitungulia 2-0 na Simba
MUIGIZAJI nyota wa filamu nchini, Shamsa Ford ambaye alimwaga chozi wakati Yanga ikikandikwa mabao 2-0 na Simba, amesema hakuwa anaigiza 'kilio' isipokuwa uchungu wa kipigo ndiyo uliomfanya amwage machozi hadharani.
Shamsa, amesema yeye ni shabiki na mpenzi mkubwa wa Yanga kiasi kwamba amekuwa hakosekani kwenye mechi zao na kipigo hicho toka kwa Simba kilimuuma na kinaendelea kumuuma isivyo kawaida.
"Mungu wangu, kuna watu wamenipiga picha! Jamani...Ni kweli kipigo kiliniliza na kinaendelea kuniuma mpaka sasa...kwa nini iwe kwa Yanga tu kila mara," alihoji Shamsa.
Muigizaji huyo ambaye anatamba kwa sasa na filamu ya 'Chausiku' alisema mpaka sasa hajui kitu gani kilichoikuta Yanga kwenye uwanja wa Taifa katika pambano la Nani Mtani Jembe la kucharazwa mabao 2-0 ikiwa ni mara ya pili baada ya mwaka jana kunyukwa mabao 3-1.
Shamsa ni miongoni mwa waigizaji walio mashabiki wa Yanga, wengine ni Vincent Kigosi 'Ray' ambaye alikuwa na wakati mgumu juu ya matokeo hayo baada ya 'kupinga' na jacob Stephen Jacob 'JB' ambayer ni mnazi wa kutupwa wa Simba.

No comments:

Post a Comment