STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 17, 2014

Waziri Ghasia akomaa, awafuta kazi wa chini yake

WAZIRI  wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu, Hawa Ghasia ametangaza kuwafuta kazi Wakurugenzi wa sita na wengine watano kuwasimamisha kutokana na matukio ya kuvurugwa kwa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji uliofanyikja Jumapili.
Pia Waziri Ghasia alisisitiza kuwa hawezi kujiuzulu kwa uzembe huo uliotia doa uchaguzi huo na badala yake amewaadhibu wa chini yake na jukumu la kujiuzulu analiacha kwa mamlaka iliytomteua licha ya kukiri uzedmbe uliofanywa na wasaidizi wake umelitia hasara taifa..
Akizungumza leo jijini Dar, Waziri Ghasia aliwataja wakurugenzi waliofutwa kazi ni Benjamin A Majoya aliyekuwa Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Mkuranga, Mkurugenzi Mtendaji wa Kaliua, Abdallah Ngodi, Masalu Mayaya wa Kasulu, Goody Pamba wa Serengeti, Julisu Madiga wa Sengerema na Simon Mayeye wa Bunda.
Wakurugenzi waliosimamishwa kazi ni Felix Mabuiga wa Hanang', Fortrunatus Fwema wa Mbulu, Isabela Chilumba wa Ulanga, Pendo Malabeja wa Kwimba na William Shimwela wa Sumbawanga Manispaa.
Waziri Ghasia alisema waliosimamishwa ni sababu ya kupisha uchunguzi na waliofutwa watapangiwa kazi nyingine za taaluma zao na kuongeza wakurugenzi wengine watatu wamepewa onyo kali.
Walioonywa niu Mohammed Maje wa Rombo, Hamis Yuna wa Busega na Ilala, Mvomero na Hai.
Uchaguzi huo uliofanyika Jumapili ulikumbwa na dosari mbalimbali zikiwamo kucheleweshwa kwa vifaa vya kupigia kura, karatasi kuwa na kasoro mbalimbali na kukwamisha kufganyika kwa uchaguzi kwa baadhji ya maeneo na kwingine kurudiwa.

No comments:

Post a Comment