STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 17, 2014

TANZIA! Mnenguaji Aisha Madinda afariki Dar

image
Aisha Madinda enzi za uhai wake
TASNIA ya sanaa imezidi kupata majozi baada ya aliyekuwa mnenguaji wa bendi za African Stars 'Twanga Pepeta' na Extra Bongo, Aisha Mohammed Mbegu 'Aisha Madinda' amefariki dunia mchana huu akiwa ndani ya Bajaj wakati akiwahi hospitali ya Mwananyamala.
Taarifa ambazo MICHARAZO imezipata zinasema kuwa Aisha Madinda alikodisha Bajaj na wakiwa kwenye foleni alikumbwa na mauti na mwili wake kwa sasa upo hospitali ya Mwananyamala ukiwa umehifadhiwa.
Akiongea na EATV Mkurugenzi wa bendi ya Twanga Pepeta amesema kuwa alipewa taarifa na daktari mmoja kuwa wameona kama mwili wa Aisha Madinda hospitalini hapo, ndipo akatuma watu kwenda kuangalia akiwemo Luiza Mbutu ili kuhakikisha kama kweli ni yeye ndipo walipogundua ni yeye.
“Mimi nipo njiani natoka Kigoma kuja Dar es Salaam, ni habari ya kusikitisha sana maana Aisha amefariki katika mazingira ya kutatanisha sana, jana alikuwa mzima na anachati na watu kwenye simu leo napigiwa simu mwili wake umekutwa umehifadhiwa kwenye hospitali ya Mwananyamala, hata sielewi nini kimetokea,” amesema Asha Baraka.
Hata hivyo taarifa ambazo hazijathibitishwa zinadai kuwa Madinda aliita dereva wa bajaj nma kuomba apelekwe Mwananyamala Hospitali na kukumbwa na mauti njiani bila dereva kujua mpaka akiwa hospitalini hapo.
Inaelezwa kuwa msiba wa marehemu Aisha uko Kigamboni na huenda akazikwa kesho huko huko.
MICHARAZO inaendelea kufuatilia na kitakachopatikana tutawafahamisha zaidi juu ya msiba huu ambao umekuja siku mooja tu baada ya Mkongwe Shem Ibrahim Karenga kufariki na kuzikwa jana jijini Dar.

No comments:

Post a Comment