STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, December 17, 2014

Sikinde yapangua safu ya uongozi, Hemba 'aula'

BENDI kongwe ya muziki wa dansi nchini, Mlimani Park 'Sikinde' imepangua safu yake ya uongozi kwa kuunda Kamati Maalum inayoongozwa na wanamuziki watatu wa bendi hiyo.
Akizungumza na MICHARAZO, Katibu wa Kamati hiyo ya bendi, Abdallah Hemba alisema kuwa karibu mwezi mzima sasa bendi yao imepangua safu ya uongozi na kuunda kamati ambayo anaiongoza yeye na wenzake wawili.
Hemba alisema viongozi wenzake wanaoiongoza Sikinde ni mcharaza gitaa mahiri, Mjusi Shemboza na Ally Jamwaka.
"Kwa sasa Sikinde inaongozwa na Kamati maalum ambayo naiongoza mimi na akina Mjusi Shemboza na Ally Jamwaka," alisema Hemba ambaye ni muimbaji mahiri wa bendi hiyo.
Katika hatua nyingine, Hemba alisema kwa sasa bendi yao inasikiliza ofa toka kwa waratibu wa muziki kwa ajili ya shoo na mahasimu wao Msondo Ngoma.
"Bado hakuna hakika kama tutafanya shoo na Msondo ili tunasikiliza ofa, sisi tupo tayari wakati wowote kupambana na wapinzani wetu," alisema Hemba mmoja ya wanamuziki  waandamizi wa bendi hiyo iliyoanzishwa rasmi mwaka 1978.

No comments:

Post a Comment