STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, December 4, 2014

Hatari! Cameroon, Ivory Coast kundi moja AFCON 2015

Results of the Orange AFCON 2015 draw
SHIRIKISHO la Soka Afrika, CAF, imetangaza droo ya makundi ya Fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (Afcon) itakayofanyika mwakani nchini Equatorial Guinea kwa kuziweka kundi moja timu za Ghana, Algeria, Afrika Kusini na Senegal.
Kwa mujibu wa droo iliyofanywa usiku wa jana, timu hizo zimewekwa kundi moja la C ambalo ni la kifo kama lilivyo kundi D lenye timu za Ivory Coast, majirani za Cameroon, Guinea na Mali.
Makundi mengine mawili ya A na B yanaonekana siyo ya kutisha ingawa timu zote 16 zitakazochuana kwenye fainali hizo za mwakani zinapewa nafasi sawa ya kutwaa ubingwa huo ambao hauna mwenyewe baada ya Nigeria kuvuliwa hatua ya makundi.
Katika Kundi A zimepangwa timu wenyeji Equatorial Guinea sambamba na Burkina Faso, Gabon na Congo, huku Kundi B likiwa na timu za zambia, Tunias, Cape Verde na DR Congo.
Fainali hizo zinatarajiwa kuanza kuchezwa Januari 17 na kufikia tamati kwa bingwa kufahamika Februari 8.

No comments:

Post a Comment