STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, December 15, 2014

Liverpool wapewa Waturuki, Ligi Ndogo ya Ulaya

http://www1.pictures.zimbio.com/gi/Andre+Wisdom+BSC+Young+Boys+v+Liverpool+FC+DEcmweK_E8Sl.jpg 
KLABU ya Liverpool ambayo ilichemsha katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya imepewa timu ya  Besiktas ya Uturuki katika hatua ya timu 32 bora ya michuano hiyo kwenye ratiba iliyopangwa leo. 
Timu zingine zilizoondoshwa katika michuano hiyo ni pamoja na Ajax Amsterdam ambao wamepangiwa kucheza na Legia Warsaw, Anderlecht wao wakipangwa na Dinamo Moscow huku Sporting Lisbon wao wakiwa wenyeji wa Wolfsburg. 
Katika mechi zingine zitazikutanisha timu za AS Roma dhidi ya Feyenoord, Inter Milan wao watacheza na Celtic, Tottenham Hotspurs dhidi ya Fiorentina wakati Athletic Bilbao wao watakuwa wenyeji wa Torino. 
Mechi za mkondo wa kwanza za michuano hiyo zinatarajiwa kuchezwa Februari 19 huku zile za marudian zikitarajiw akuchezwa Februari 26.

No comments:

Post a Comment