STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 5, 2015

Azam yafufuka Zanzibar yainyoa KMKM

AZAM FC imezidnuka kwenye michuano ya Kombe la Mapinduzi baada ya kupata ushindi mwembamba wa bao 1-0 dhidi ya Mabingwa wa Zanzibar, KMKM katika mechi iliyochezwa usiku wa jana kwenye uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Bao pekee la Azam liliwekwa kimiani katika dakika ya 18 kutokana na kujifunga kwa nahodha wa KMKM, Khamis Ali akijaribu kuokoa mpira wa krosi ya Shomari Kapombe.
Ushindi huo umeifanya Azam kufikisha pointi 4 na kulingana na timu ya KCCA waliotoshana nao nguvu katika mechi yao ya kwanza walipofungana mabao 2-2.
Michuano hiyo inatarajiwa kuendelea leo kwa michezo ya Kundi C Mafunzo wakivaana na Mtibwa Sugar majira ya saa 10:00 jioni uwanja wa Amaan kabla ya usiku Simba watashuka dimbani kuchuana na JKU.

No comments:

Post a Comment