STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, January 5, 2015

Fernando Torres atambulishwa Atletico Madrid baada ya kurejea

2
Torres alipotambulishwa klabu ya Atletico Madrid
3456MSHAMBULIAJI nyota wa zamani wa Liverpool na Chelsea, Fernando Torres amerejea rasmi kwenye klabu yake ya zamani ya Atletico Madrid ya nchini Hispania.
Torres aliondoka miaka saba iliyopita kwa kujiunga na Liverpool ya England kabla ya kuhamia Chelsea na baadauye kutolewa kwa mkopo AC Milan.
”Nimefurahi sana kurejea klabu yenye nafasi kwenye maisha yangu,niliondoka kwenye klabu hii kwenda kukuza kiwango changu,nafurahi kurejea tena Atletico ikiwa sasa inashindana na vilabu vikubwa ulimwenguni,nimerejea kushinda na mataji na klabu hii niipendayo”.
Hayo yalikuwa maneno ya Torres wakati akizungumza na waandishi wa habari wakati wa utambulisho wake uliohudhuliwa na mashabiki zaidi ya 45,000 kwenye dimba la Vicente Calderon jana.

No comments:

Post a Comment