STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 11, 2015

Mgambo JKT yaitoa nishai Ruvu Shooting Mkwakwani


http://tplboard.co.tz/assets/uploads/files/273f8-63.jpg
Mgambo JKT waliopata ushindi dhidi ya Ruvu Shooting
TIMU ya Mgambo JKT imeitoa nishai Ruvu Shooting katika mfululizo wa Ligi Kuu Tanzania Bara mchezo pekee uliochezwa  leo kwenye uwanja wa Mkwakwani Tanga baada ya kuicharaza bao 1-0.
Ruvu Shooting inayonolewa na kocha Mkenya, Tom Oloba ilishindwa kuhimili vishindo vya maafande wenzao licha ya tambo zilizokuwa zikitolewa na uongozi wa klabu hiyo chini ya Msemaji wao, Masau Bwire.
Bao hilo la wenyeji liliwekwa kimiani na Full Maganga katika dakika ya 44, likiwa ni bao la kwanza kwa mchezaji huyo ambaye amekuwa na kismati cha kuzitungua Simba na Yanga.
Kwa ushindi huo Mgambo imefikisha pointi 12 na kuchupa kutoka nafasi ya 12 hadi nafasi ya nane wakiing'oa Ruvu Shooting ambayo imesaliwa na 11.
Msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara baada ya mchezo wa leo:
                                 P   W    D    L    F    A   GD   Pts
01. Mtibwa Sugar       08  04  04  00  11  04  07   16
02. JKT Ruvu             10  05  01  04  10  09   01  16
03. Yanga                  08  04  02  02  11  07   04  14
04.  Azam                  08  04  02  02  10  06   04  14
05.  Kagera Sugar      09  03  05  01  07  04   03  14
06.  Polisi Moro          10  03  05  02  09  08   01  14
07. Coastal Union      09  03  03   03  09  08   01  12
08.  Mgambo JKT      09  04  00  05   05    09  -4  12
09. Ruvu Shooting    10  03  02   05   05   08  -3  11
10. Stand Utd           10  02  05   03   07   12  -5  11
11. Ndanda Fc          10  03  01   06  10    14  -4  10
12. Simba                08  01  06   01   07   07  00  09
13. Mbeya City         08   02  02   04  03   06  -3   08
14. Prisons               09  01  04   04  06   08  -2   07

Wafungaji Bora:
5-
Didier Kavumbagu(Azam)
4-
Rama Salim (Coastal), Danny Mrwanda, Simon Msuva (Yanga) Ame Ally (Mtibwa), Samuel Kamuntu (JKT Ruvu)

3- Ally Shomari, Emmanuel Okwi (Simba), Rashid Mandawa (Kagera Sugar), Jacob Massawe (Ndanda)
2- Shaaban Kisiga, (Simba), Nassor Kapama (Ndanda) Salum Kanoni (Kagera), Aggrey Morris (Azam),  Najim Magulu, Jabir Aziz (JKT Ruvu), Amissi Tambwe, Jerry Tegete (Yanga), Ibrahim Kihaka (Prisons), Mussa Mgosi (Mtibwa), Heri Mohammed, Mussa Said (Stand Utd), Ally Nassor (Mgambo),  Malimi Busungu (Mgambo), Nicolaus Kabipe (Polisi)
1- Joseph Owino (Simba), Coutinho, Kelvin Yondan, Haruna Niyonzima, Jaja (Yanga), Deo Julius, Steven Mazanda (Mbeya City), Bakari, Imani Mapunda, Said Bahanuzi (Polisi-Moro), Kipre Tchetche,  Aggrey Morris, SHomar Kapombe, John Bocco  (Azam), Ernest Joseph, Paul Ngalema,  (Ndanda), Jacob Mwaitalako,  Laurian Mpalile, Amir Omary, Hamis Mahingo (Prisons), Lutimba Yayo, Kennedy Masumbuko, Joseph Mahundi, Hussein Sued,Itubu Intembe (Coastal), Ramadhani Pella, Full Maganga (Mgambo), Said Mkopi, Vincent Barnabas (Mtibwa), Amos Mgina, Najim Magulu, (JKT Ruvu), Salum Kamana, Shaaban Kondo (Stand Utd), Paul Ngwai, Atupele Green(Kagera Sugar), Juma Nade, Abdulrahman Mussa, Thomas Mathayo , Hamis Kasanga ,Zubeiry Dabi (Ruvu Shooting)

No comments:

Post a Comment