STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, January 11, 2015

Inter Milan yatamba nyumbani,

Nemanja Vidic
Vita ya Inter Milan dhidi ya Genoa leo
KLABU ya Inter Milan imefanikiwa kuifumia Genoa kwa kuicharaza mabapo 3-1 katika mechi kali ya Ligi Kuu ya Italia, Serie A, wakati AS Roma na mahasimu wao Lazio wametoshana nguvu ya maba0 2-2.
Inter ikiwa nyumbani ilipata ushindi huo kupitia mabao ya Palacio katika dakika ya 12, Mauro Icardi dakika ya 39 na Nimanja Vidic dakika mbili kabla ya mechi kumalizika, huku bao la wageni lilifungwa na Izzo dakika ya 85.
Katrika mechi nyingine za ligi hiyo,
Atlanta ikiwa nyumbani imelazimishwa sare ya 1-1 na Chievo Verona, Cagliari ikainyoa Cesena mabao 2-1 na Fiorentina ikipata ushindi mtamu nyumbani dhidi ya Palermo baada ya kuinyoa mabao 4-3.
Nayo Hellas Verona ikiitafuna Parma waliowafuata kwao kwa mabao 3-1 na Mahasimu wa jiji la Roma, AS Roma na Lazio zilishindwa kutambiana kwa kutoka sare ya 2-2 na Sampdoria iliilaza Empoli kwa bao 1-0 baadaye Napoli watakuwa wenyeji wa vinara Juventus.

No comments:

Post a Comment