STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 25, 2015

John Riise athibitisha kumuaga Gerrard

http://sillyseason.com/sites/default/files/styles/article_top/public/article_images/riise_gerrard_reut960_1212152704.jpg?itok=zL9GLXlT
Riise akiwa na nahodha wake wa zamani, Gerrard
John Arne Riise enzi akiitumikia Liverpool
LONDON, England
BEKI wa kushoto wa zamani wa kimataifa wa Norway, John Arne Riise amethibitisha kushiriki pambano maalum la kumuaga Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard akiungana na nyota wengine wa klabu hiyo ya Anfield.
Mechi hiyo maalum inatarajiwa kuchezwa Machi 29 kwenye uwanja wa Anfield, ikiwarejesha nyota wa zamani wa Liverpool waliwahi kucheza na nahodha huyo ili kuaga kabla ya mwanasoka huyo wa kimataifa wa Uingereza ajahamia klabu yaLA Galaxy ya Marekani mwishoni mwa msimu huu.
Kupitia akaunti yake ya Instagram, Riise alithibitisha kuwa atakuwa miongoni mwa watakaokuwapo Anfield kumuaga Gerrard katia pambano hilo litakalohusisha kikosi cha sasa cha Liverpool na kikosi cha zamani cha mabingwa hao wa zamani wa England na Ulaya.
Nyota wengine watakaoshiriki pambano hilo ni Fernando Torres 'El Nino', Xabi Alonso, Pepe Reina, Javier Mascherano na Luis Suarez ambao wameshathibitisha kucheza pambano hilo, huku Riise akimtaja pia Luis Garcia naye atakuwapo.
"Najisikia fahari kubwa kwa kuwalikwa kwenye pambano la hisani la Steven Gerrard la Machi 29, sio la kusubiri kushuhudia magwiji waliocheza pamoja kushuka tena dimbani ," aliandika Riise.

No comments:

Post a Comment