STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 25, 2015

Simba, Yanga zavuna zaidi ya Sh. Mil. 100 viwanja vya ugenini


Kikosi cha Simba
Kikosi cha Yanga
KLABU za Simba na Yanga zimeingiza jumla ya Sh. Mil. 100 katika mechi zao za mwishoni mwa wiki viwanja vya ugenini.
Pambano lililowakutanisha wenyeji timu ya Stand United kwenye Uwanja wa Kambarage mjini Shinyanga dhidi ya timu ya Simba umeingiza jumla ya Sh. Mil.31.
Jumla la watazamaji 5,439 waliingia uwanjani kushuhudia mchezo huo, ambao timu ya Stand imepata mgao wa Sh. 6,564,268.22 na Simba wakipata mgao wa 4,661,581.78.
VAT (18%) tshs. 4,763,135.59 huku FA  mkoa wakipata tsh.665,940.25, FDF tsh. 1,141,611.86, Bodi ya Ligi tsh. 1,522,149.15, Gharama za mchezo tsh. 1,617,283.47, Uwanja tsh. 2,854,029.66, Gharama ya tiketi tsh. 1,593,000,00, FDF tsh. 2,921,000.00, TFF tsh.2,921,000.00
Wakati kwenye uwanja wa Sokoine Mbeya, jumla ya Sh. 74, 600,000.00, zilipatikana kutokana na watazamaji 14,920 waliokata tiketi kushuhudia mchezo huo, lililozihusisha wenyeji Mbeya City na Yanga.
Kwa mujibu wa mgao VAT(18%) tsh.11,379,661.02, CDRB (5%) tsh.3,730.000.00, FDF tsh. 5,222,000,00, TFF tsh. 2,238,000.00, Uwanja tsh. 7,804,550,85, Gharama za mchezo tsh 4,442,578.81, Bodi ya Ligi tsh. 4,162,427,12.
Chama cha soka mkoa (FA) Mbeya kimepata tsh. 1,821,061.86, FDF(TFF) tsh. 3,121,820.34, wenyeji timu ya Mbeya city wakipata tsh. 17,950,466.95 na klabu ya Yanga tsh. 12,747,438.98.

No comments:

Post a Comment