STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 25, 2015

Kocha Spurs awaonya nyota wake pambano la Fiorentina

KOCHA wa Tottenham Hotspur, Mauricio Pochettino amewaonya wachezaji wake akiwataka kuichukulia pambano lao la marudiano ya Ligi Ndogo ya Ulaya wakiwa ugenini dhidi ya Fiorentina ya Italia kama pambano la fainali.
Pochettino amewataka wachezaji wake wasiweke akili zao kwa pambano la Fainali za Kombe la Ligi (Capital One) dhidi ya Chelsea litakalochezwa Jumapili kwenye uwanja wa Wembley na kujisahau mbele ya Fiorentina iwapoa wanataka kutinga 16 Bora.
Spurs itavaana Chelsea kwa mara ya kwanza kwenye uwanja wa Wembley tangu mwaka 2008 na kocha huyo amesisitiza wachezaji wake waelekeze nguvu kwa pambano hilo lakini wasisahau 'fainali' nyingine dhidi ya Fiorentina ambao walitoka nao sare ya 1-1 wiki iliyopita.
Pochettino alisema: Alhamisi (leo) litakuwa pambano gumu mno. Nafikiri itakuwa ni fainali ya kwanza kwetu kabla ya Jumapili, Fiorentina ni timu pekee ambayo itaweza kutuvusha hatua nyingine ya michuano ya Ligi Ndogo ya Ulaya."
"Tunajua tunahitajika kufunga baada ya sare ya 1-1 na tunajiamini. Tunajiamini na tunapaswa kuchukua tahadhari kwa mchezo hio wa Alhamisi. Tunapaswa kupambana ili tushinde na wachezaji wanapaswa kufanya hivyo," alisema kocha huyo kuyoka Argentina.
Kocha huyo aliongeza kuwa; "Hii ni fainali nyingine na tunahitaji kufanya maamuzi (ya nani acheze) kwa sababu tumetoka kucheza mechi ngumu dhidi ya Fiorentina na West Ham,".
Spurs ambao mwishoni mwa wiki walinusurika kipigo nyumbani kwa kutoka nyuma na kurudisha mabao mawili dhidi ya West Ham Utd na kutoka sare ya 1-1 watavaana na Fiorentina katika mjini ya Frolence wakihitajika kushinda au kupata sare ya mabao zaidi ya mawili ili kutinga 16 Bora ya michuano hiyo ambayo leo pi itashuhudiwa mechi kadhaa za marudiano kabla ya kujulikana timu 16 zitakazosonga mbele.
Mojha ya pambano linalosubiwa kwa hamu ni lile la Liverpool dhidi ya Besiktas ya Uturuki ambao katika mechi ya mkondo wa kwanza uwanja wa Anfied, Liverpool ilishinda bao 1-0 la mkwaju wa penati ya 'kulazimisha' ya Mario Balotelli.

No comments:

Post a Comment