STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Wednesday, February 25, 2015

Luis Enrique kuendelea kumtumaini Messi katika penati

Joe Hart
Joe Hart akiojkoa mkwaju wa penati ya Messi usiku wa jana
Lionel Messi watches on as Hart does brilliantly to save his last-minute penalty  
Messi akiwa haamini kama mkwaju wake umezuiwa na kipa wa Man City
Hart celebrates saving the last-gasp penalty as Pedro holds his head in his hands and Messi lies on the floor
Messi akiwa amelala chini baada ya kukosa penati
MENEJA wa klabu ya Barcelona, Luis Enrique amesisitiza kuwa Lionel Messi ataendelea kuwa mpiga penati wa timu hiyo pamoja na kukosa penati yake ya nne msimu huu katika mchezo dhidi ya Manchester City juzi.
Nyota huyo wa kimataifa wa Argentina alikuwa na nafasi ya kuipa ushindi Barcelona wa mabao 3-1 katika dakika za majeruhi lakini Joe Hart alifanikiwa kuokoa mchomo wake.
Messi pia amekosa penati katika mchezo dhidi ya Levante, Septemba mwaka jana na Brazil wakati akiitumikia timu yake ya taifa Oktoba lakini Enrique anaamini kuwa nyota huyo bado ni mpigaji mzuri na anamuamini.
Kocha huyo amesema wale wote wanaokosa penati ni wale wenye uthubutu wa kufanya hivyo na Messi bado ataendelea kuwa mpigani wao.
Katika mchezo huo wa mkondo wa kwanza uliofanyika katika Uwanja wa Etihad, Barcelona ilifanikiwa kupata ushindi wa mabao 2-1, ikiwa ni siku chache ikitoka kupokea kipigo cha bao 1-0 nyumbani Camp Nou dhidi ya Malaga katika Ligi Kuu ya Hispania (La Liga).
Kukosa penati hiyo ya juzi imemfanya Messi kulingana na Cristiano Ronaldo, Luis Figo and Andy Shevchenko katika michuano hiyo ya Ulaya wakitanguliwa na Ruud Van Nistelrooy aliyekosa mabao manne na Thierry Henry anayeongoza kwa kukosa penati tano.
Pia ni penati ya 13 kwa mkali huyo wa mabao wa Cataluna kati ya mikwaju 59 aliyopiga akiwa na klabu ya Barcelona, huku kwa upande wa nchi yake ya Argentina Messi amekosa mbili kati ya 12 alizopiga

No comments:

Post a Comment