STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 15, 2015

Kagera Sugar wazipumulia Azam, Yanga

http://api.ning.com/files/cPakA0chAEyfyqjZRP3k2djpZ9GyxNW23W69D7FY4fYhsuNz2vmH6gr7yEITcci18IdnTvIgOej4xydmYu8LtJiXW0uQDhCL/16.jpg
Kagera Sugar walioifyatua JKT Ruvu
BAO pekee la dakika ya 38 lililofungwa na kiungo mshambuliaji wa zamani wa Yanga na Coastal Union, Atupele Green limeiwezesha Kagera Sugar kuichapa JKT Ruvu na kuchupa hadi nafasi ya tatu ikizipumulia timu za Azam na Yanga zinazoongoza msimamo wa Ligi Kuu Tanzania Bara.
Kagera ilipata ushindi huo kwenye uwanja wa Kambarage-Shinyanga baada ya kuilaza maafande hao wa JKT kwa bao 1-0.
Ushindi huo ni wa pili mfululizo kwa timu hiyo kwenye uwanja huo tangu walipohamia wakitokea CCM Kirumba walipokuwa wakiambulia vipigo mfululizo.
Kwa ushindi huo Kagera imefikisha pointi 21 na kushika nafasi ya tatu, pointi nne nyuma ya Azam na Yanga wanaongoza wakiwa na pointi 25 ingawa timu hizo mbili zina michezo miwili mikononi zaidi ya Kagera.
Kagera wenyewe wamecheza michezo 15 wakati Azam na Yanga wamecheza mechi 13 tu ingawa katikati ya wiki hii watakuwa viwanja kucheza viporo vyao.
Simba wamechupa nafasi ya nne baada ya kuisulubu Polisi Moro mabao 2-0 uwanja wa Jamhuri Morogoro kwa kufikisha pointi 20 baada ya mechi 14.
MSIMAMO LIGI KUU TZ BARA 2014-2015
                              P   W   D    L    F    A   GD  Pts
01.  Yanga              13  07  04  02  15  07  08   25
02.  Azam               13  07  04  02  22  12  10   25
03. Kagera Sugar    15  05  06  04  12  11  01   21
04. Simba               14  04  08  02  15  11  04   20
05. Mtibwa Sugar    14  04  07  03  15  14  01   19
06. Polisi Moro        15  04  07  04  12  13   -1   19
07. Coastal Union   15  04  07  04  11   10  01   19
08. JKT Ruvu          15  05  04  06  14   15  -1   19
09. Ruvu Shooting  14  05  04  05  10   11  -1   19
10. Mbeya City       14  04  05  05   09   11  -2   17
11. Ndanda Fc        15  04  04  07   13   18  -5   16
12. Stand Utd         15  03  06  06   13   18  -5   15
13. Mgambo JKT     13  04  02  07   07   15  -8   14
14. Prisons             13  01  08   04   10   12  -2  11
Wafungaji:

 8- Didier Kavumbagu(Azam)
6-
Samuel Kamuntu (JKT Ruvu), Ame Ali (Mtibwa), Rashid Mandawa (Kagera Sugar)
 

5-Danny Mrwanda (Yanga), Kipre Tchetche (Azam)
 

4- Rama Salim (Coastal),  Simon Msuva (Yanga),  Emmanuel Okwi (Simba), Nassor Kapama (Ndanda), Heri Mohammed (Stand Utd)
 

3- Ally Shomari (Mtibwa),  Jacob Massawe (Ndanda),Frank Domayo (Azam), Malimi Busungu (Mgambo), Achidilele (Stand Utd), Atupele Green (Kagera)

No comments:

Post a Comment