STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 15, 2015

AZAM YAIFYATUA EL MERREIKH 2-0

Azam waliowapa raha Watanzania leo Chamazi
MABINGWA wa soka nchini Azam wameanza vyema michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika baada ya kuifumua El Merreikh ya Sudan kwa mabao 2-0 katika pambano la awali la mkondo wa kwanza lililochezwa uwanja wa Chamazi, Dar es Salaam.
Ushindi huo umekuwa siku moja tu baada ya wawakilishi wengine wa Tanzania katika Kombe la Shirikisho Yanga, kupata ushindi kama huo dhidi ya BDF XI ya Botswana, shukrani zikienda kwa Mshambuliaji wa Kirundi, Amissi Tambwe aliyefunga mabao yote mawili katika kila kipindi jana.
Mabao ya washindi yalifungwa na Didier Kavumbagu na John Bocco Ádebayor' katika kila kipindi na kuifanya Azam kuendeleza rekodi yake katika michuano ya kimataifa kwa kutoruhusu kipigo katika uwanja wa nyumbani dhidi ya wapinzani wao.
Ushindi huo pia kumeiweka Azam katika nafasi nzuri kwa mechi ya marudiano wiki mbili zijazo, inagwa Azam haipaswi kubweteka kwa ushindi huo.

No comments:

Post a Comment