STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, February 15, 2015

Toto Afrika, Mwadui zarudi Ligi Kuu 2005-2016

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEgaPRe88ZbguLMay9hq8z-MrwZbKRJuuDlKpnOd2wtCCvgsjqCFEWatffl7Dv95XsNWxsZcZutmnogqEcrMxCmWUYaFQlW7HdciyoGr9TrkJealnP3YNu3bp8bM8-sqrTXkYziW61qIkaiy/s1600/TFF+Toto+Africans.jpg
Toto Africans
http://taarifa.co.tz/wp-content/uploads/2015/01/DSC_4165.jpg
Mwadui Shinyanga waliopanda Ligi Kuu
TIMU za Toto Africans na Mwadui Shinyanga zimeungana na timu za Majimaji-Songea na Africans Sports kurejea Ligi Kuu Tanzania Bara msimu ujao baada ya kupata ushindi katika mechi zao za kufungia msimu wa Ligi Daraja la Kwanza Tanzania Bara zilizochezwa mikoa ya Mwanza na Shinyanga.
Toto ilipata ushindi wa mabao 2-0 dhidi ya Rhino Rangers ya Tabora wakati Mwadui imeishindilia Burkina Faso kwa mabao 4-3 na kuungana na Majimaji Songea na Africans Sports zilizotangulia mapema kurejea ligi kuu.
Timu hizo zote nne zilizopanda daraja ziliwahi kucheza Ligi Kuu kwa nyakati tofauti, huku Majimaji na Africans Sports zikiwahi kuwa mabingwa miaka tofauti kabla ya kuporomoka hadi madaraja ya chini.

No comments:

Post a Comment