STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 6, 2015

Berry Black ajiunga Mkubwa na Wanae atoa 'Byebye'

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEihS4zZARw-TfuBJsdn2gLhVxk0_0S7PM1Osw6yjrHX153vcpTeVQpNfb9Hz2xO_CNqAUi5ySCsVlj4JsJXCsSLvM_lmIEDHoKdGDnYfPP5svuamSbQ7jWLS6IPpjXBIVrJEAx2JcY__i8/s1600/photo+%252818%2529.JPG
Berry Black
MSANII nyota wa zamani wa kundi la 2 Berry, Berry Black amejiunga na 'lebo' ya Mkubwa na Wanae na tayari ametengeneza ngoma mpya iitwayo 'Byebye' alioimba akiwashirikisha wasanii wa Yamoto Band, Maromboso na Aslay.
Akizungumza na MICHARAZO, Mkurugenzi wa Kituo cha Mkubwa na Wanae, Said Fella alisema kuwa, msanii huyo ameingia mkataba wa kufanya kazi chini ya lebo yao na wamesharekodi wimbo mmoja uliotokana sambamba na video yake.
Fella alisema wimbo huo wa 'Byebye' umetengenezwa katika studio za Vibe Records chini ya mtayarishaji wake, Shirko na video imetengenezwa kupitia kampuni ya Kwetu Studio chini ya Msafiri Shaaban.
"Tumeamua kumrejesha hewani Berry Black kwa kumchukua Mkubwa na Wanae na tumeshatengeneza kazi moja ya 'Byebye' aliyoimba na madogo wa Yamoto na tutaiachia hadharani Ijumaa (leo) audio na video yake," alisema Fella.
Fella alidokeza kuwa baada ya kufanya utambulisho wa kazi hiyo ya Berry Black visiwani Zenji wakisindikiza onyesho la Yamoto Band, wataanza mipango ya kumtoa hadharani Ferooz nyota wa zamani na muasisi wa Daz Nundaz ambaye naye yupo Mkubwa na Wanae ambaye amesharekodi nyimbo mbili ambazo hakutaja majina yake

No comments:

Post a Comment