STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, March 6, 2015

Yamoto Band kupeleka za uzunguni Zenji

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEhdD6fCyy7ZBqhFtxtqvW5KpIIwHWzTVxWC8ihmF-NkUM-D0pXao8M7JfLrwK7djE5X5N3mWgOIuauilu7bH-Do-ghMxGXiA0Y5a4DH8oSeGyOGLbxMeun64ypd3T4AmQDqVXwRxUQepsy9/s1600/IMG_20150107_010322.jpgBAADA ya kurejea kutoka Uingereza walipoenda kutumbuiza mjini London kundi la Yamoto Band linatarajiwa kwenda kuonuyesha makali ya ugahibuni visiwani Zanzibar Jumapili hii.
Mkurugenzi wa kundi hilo, Said Fella aliliambia MICHARAZO kuwa, Yamoto wataenda kutambulisha nyimbo zao mpya na ubunifu waliotoka nao kwa Malkia katika onyesho litakalofanyika Ngome Kongwe, visiwani humo.
Fella alisema onyesho hilo litasindikizwa na wasanii mbalimbali kutoka TMK na wale wa visiwani humo.
"Tumerejea juzi kutoka Uingereza na Jumapili tunatarajiwa kuvuka maji kwenda Zanzibar kwa ajili ya uitambulisho wa mambo mapya ya Yamoto Band, onyesho litafanyika Ngome Kongwe na kusindikizwa na wasanii mbalimbali.
Katika hatua nyingi msanii Nikki Mbishi aliyetangaza hivi karibuni kuachana na fani ya muziki amevunja ukimya kwa kuibuka na wimbo uitwao 'Sihusiki nao' akimshirikisha mshindi wa BSS 2013, Walter Chilambo.
Nikki alitangaza kuachana na muziki na kuibua mjadala mkubwa ambao ulisababisha kushambuliwa na baadhi ya marapa wenzake wakidai 'amechemsha'.

No comments:

Post a Comment