STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 15, 2015

HAKUNA UFISADI UNUNUZI KIVUKO CHA MV DAR ES SALAAM

Mtendaji Mkuu wa TEMESA, Eng. Mercelin Magesa
WAKALA wa Ufundi na Umeme (TEMESA) umesema hakuna ufisadi wowote ambao umefanyika katika mchakato mzima wa ununuzi wa Kivuko cha Mv Dar es Salaam.
Kauli hiyo Temesa imetolewa na Mtendaji Mkuu wa wakala huo Mhandisi Marcelin Magesa ikiwa ni siku moja baada ya Wajumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu kuilalamikia Serikali kwa uamuzi wake wakununua Kivuko hicho wakati hakina tija kwa jamii.
Magesa alisema maandalizi ya awali ya ununuzi wa Kivuko hicho yalishirikisha wadau wote ambapo lengo lake ni kutoa huduma ya usafiri wa majini katika ukanda wa bahari ya Hindi.
Mtendaji Mkuu huyo alisema mpango wa ununuzi wa Kibuko hicho uliwasishwa katika Bunge la Bajeti la mwaka 2012/13 ambapo ulitengewa fedha ambapo fedha zingine zilitengwa bajti ya 2013/14 na 2014/15.
"Napenda kuweka wazi suala hili kwani juzi habari zilizotoka kwenye baadhi ya vyombo vya habari zinaonesha kuwa kuna mapungufu lakini utaratibu ulifuatwa kwa kutangazwa zabuni ambapo kampuni ua Ms. Johs Gram-Hanssen ya Denmark ndio ilishinda zabuni ya ujunzi wa Kivuko hicho kwa dola za Kimarekani 4,980,000 sawa na fedha za Tanzania sh.bilioni 7.916,955,000," alisema Magesa.
Alisema ujenzi wa Kivuko cha Mv Dar es Salaam, ulifanyika hatua kwa hatua ambapo kilifanyiwa ukaguzi mara nne Novemba 2013, Februari 2014, Julai 2014 na Septemba 2014 ambapo kiliingizwa majini kufanyiwa majaribio.
Magesa alisema kutokana na utaratibu wa ukaguzi huo ni dhahiri kuwa Kivuko hicho ni kipya, na kauli kuwa sio kipya zinahitaji kupuuzwa.
Mtendaji Mkuu alisema lengo la Kivuko hicho ni kupunguza msongamano ambao umekuwa ukiongezeka katika jiji la Dar es Salaam.
Alisema kwa sasa Temesa inaendelea kutoa huduma za usafiri nchini katika vituo mbalimbali 28  ambapo tangu mwaka 2012 wamenunua vivuko vitano vipya.
Mhandisi huyo alivitaja vivuko hivyo kuwa ni Mv Kilambo, Mv Mafanikio vinavyotoa huduma Mtwara, Mv Malagarasi Kigoma, Mv Tegemeo Mwanza na Mv Dar es Salaam

No comments:

Post a Comment