STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 15, 2015

CHELSEA WANG'ANG'ANIWA NYUMBANI

BANNER-Chelses-Southampton-v5.jpg
Muunganiko wa picha zilizochapishwa na Daily Mail wakati Chelsea wakilazimishwa sare nyumbani
VINARA wa Ligi Kuu ya England, Chelsea wameshindwa kutamba nyumbani baada ya kung'ang'aniwa na Southampton na kulazimishwa sare ya bao 1-1 katika mfululizo wa ligi hiyo.
Chelsea walikuwa wa kwanza kupata bao katika dakika ya 11 kupitia bao la kichwa cha Diego Costa aliyemalizia krosi murua ya beki Branislav Ivanovic.
Dakika nane baadaye Southampton walifanikiwa kurejesha bao hilo kwa mkwaju wa penati baada ya Namanja Matic kucheza madhambi na Dusan  Tadic.
Kipa wa Chelsea aliucheza mpira huo kwa miguu, lakini kasi yake ulimzidi na kutinga wavuni na matokeo yalibaki hivyo hivyo licha ya wenyeji kucharuka na kulifikia lango la wageni wao, lakini kipa Fraser Forster alikuwa kikwazo kupata magoli ya kuwapa pointi tatu muhimu.
Hivi punde Everton watawalika dimbani Newcastle na Manchester United baadae itaikaribisha Tottenham Hotspur.

No comments:

Post a Comment