STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 15, 2015

MIZANI YA KIBAHA MWISHO JUMANNE, TANROADS KUIFUNGA

https://blogger.googleusercontent.com/img/b/R29vZ2xl/AVvXsEiBjce7YAgsA0NVXYFoM2Ych1mXqHSwidkas5I6_20N2mZC6EJHiNNxPmRIvNNdAiOhryhfMf6wxsDFE2HOfLw7Ycv9Q6qtNu6rIaTp8Cjq0wQDWtYSISXeCr2Ges8oZJ4qi29r47JqkGDT/s1600/mizani+ya+kibaha.jpgWAKALA wa Barabara Tanzania (TANROADS), umesema kuanzia Machi 17 mwaka huu mzani wa kupimia magari Kibaha hautaendelea kutoa huduma kwa magari na huduma hiyo itahamia katika mzani mpya wa Vigwazwa.
Hayo yalisemwa na Mtendaji Mkuu wa Tanroads Mhandisi Patrick Mfugale wakati akizungumza na waandishi wa habari jana jijini Dar es Salaam.
Alisema mzani wa Kibaha ulikuwa unatumia dakika moja na nusu kupima gari moja hali ambayo ilikuwa inasababisha msongamono ila mzani wa Vigwaza utakuwa unatumia sekunde 30 kwa gari moja.
Mhandisi Mfugale alisema kituo hicho cha Vigwazwa ni cha kisasa kina Mtambo wa Kuchambua magari (Weight-in- Motion) kwa kupima magari yakitembea.
Pia Mfugale alisema hicho kina Mzani Mkubwa (Multi-deck) unaweza kupima gari lolote kwa mkupuo hali ambayo itasaidia kupunguza msongamano.
"Mzani wa Vigwaza umekamilika na juzi ulianza kazi kwa majaribio ila tunatarajia kusitisha huduma ya upimaji uzito eneo la Kibaha kesho, hivyo ni vyema madereva wakajiandaa kwa hilo," alisema.
Alisema barabara ya za kuingia katika mzani huo ambazo zina kilometa 1.8 zimekamilika ambazo zina upana wa milikita 200 na kudumu kwa miaka zaidi ya 50.
Mtendaji Mkuu huyo alisema mzani huo utakuwa unaelekeza magari ambayo yamezidisha mzigo wapi yakapaki na yale ambayo hayana tatizo yaendelee kwa safari.
Alisema magari yanayotakiwa kupima uzito ni kuanzia yale yenye uzito kuanzia tani 3.5 ambapo aliwataka madereva kufuata taratibu na sheria za barabara kwa kuacha nafasi ya mita 30 kati ya gari na gari.
Mhandisi Mfugale alitoa rai kwa wamiliki wa magari kuhakikisha kuwa wanatengeneza magari yao ili kuepusha kuharibika katika eneo hilo kwani watapigwa faini.
Mfugale alisema mzani huo umegharimu bilioni 11 ambapo jitihada zao ni kuendelea na ujenzi katika mzani nyingine ili ziweze kuwa na ubora kama wa Vigwaza.

No comments:

Post a Comment