STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 15, 2015

Wenger anaamini wataing'oa AS Monaco

http://d.ibtimes.co.uk/en/full/110907/arsene-wenger.jpg
Kocha Wenger
KOCHA wa klabu ya Arsenal, Arsene Wenger anaamini kikosi chake kinaweza kuing’oa Monaco katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya pamoja na kufungwa mabao 3-1 katika mchezo wao wa kwanza. Arsenal inatarajiwa kucheza na Monaco Jumanne ijayo huku kukiwa hakuna timu ambayo ilifanikiwa kusonga mbele baada ya kipigo kama hicho katika mashindano hayo.
Akihojiwa, kocha Wenger amesema anajua changamoto kubwa iliyopo mbele yao lakini watajitahidi kufanya kila wanaloweza ili kuhakikisha wanasonga mbele.
Kocha huyo aliendelea kudai kuwa anajua Monaco wanapewa nafasi kubwa lakini wanaweza kubadili hilo kama wakitumia maarifa na ujuzi wao wote.
Ili waweze kusonga mbele Arsenal wanatakiwa walau wafunge mabao matatu huku wakijitahidi kudhibiti lango lao.
Mechi nyingine kwa siku hiyo ya Jumanne itazikutanisha timu za Atletico Madrid dhidi ya Bayer Leverkusen walioshinda nyumbani kwao bao 1-0.
Jumatano ijayo kutakuwa na mechi nyingine mbili kwa Juventus ya Italia kuwafuata Borussia Dortmund iliyolala ugenini 2-1 na Barcelona wataialika Manchester City ambao waliwafumua 2-1 katika mechi ya kwanza mwezi uliopita kwa mabao ya Luis Suarez.

No comments:

Post a Comment