STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Sunday, March 15, 2015

YANGA MPAKA RAHA, YAUA WAZIMBABWE 5-1

Tambwe ameendelea kuongeza idadi ya mabao katika michuano hiyo ya Afrika baada ya leo kufunga bao la tatu
http://www.herald.co.zw/wp-content/uploads/2015/02/ABDD.jpg
Wazimbabwe waliofumuliwa 'mkono'na Yanga kwenyue uwanja wa Taifa leo
AMA kweli Yanga ya sasa ni ya Kimataifa baada ya jioni hii kuifumua timu ya FC Platinum ya Zimbabwe kwa mabao 5-1 katika pambano la kwanza la raundi ya kwanza ya Kombe la Shirikisho Afrika.
Ikikosa huduma za nyopta wake kadhaa akiwamo nahodha, Nadir Haroub 'Cannavaro', Yanga ilipata karamu hiyo kwenye uwanja wa Taifa, Dar es Salaam na kujiweka nafasi nzuri ya kutinga raundi ya pili.
Mabao ya Salum Telela aliyekuwa nahodha wa Yanga leo uwanjani, Haruna Niyonzima, Amissi Tambwe na mawili ya 'Uncle' Mrisho Ngassa yalitosha kuwanusisha vijana wa Jangwani raundi ijayo ambayo huenda wakavaana na ama Etoile du Sahel ya Tunisia au Benfica de Luanda ya Angola.
Mpaka mapumziko Yanga walikuwa mbele kwa mabao 2-1 kabla ya kipindi cha pili kuongeza mengine na kuwapa wasaa nzuri kwa mechi ya marudiano wiki mbili zijazo, Yanga wakihitaji sare yoyote kusonga mbele.
Tofauti na ilivyotarajiwa mapema kwamba huenda Platinum waliyoing'oa Sofapaka ya Kenya kwa jumla ya mabao 4-2 ingewapeleka puta Yanga, mambo yamekuwa tofauti kwa wenyeji kuwapeleka mchakamchaka.

No comments:

Post a Comment