STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 3, 2011

Akudo Impact yanyakua wanenguaji wapya





BENDI ya Akudo Impact imeongeza nguvu kwenye safu ya ushambuliaji wa jukwaa baada ya
kuwanasa wanenguaji watatu kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo.
Kwa mujibu wa meneja wa bendi hiyo George Kyatika, wanenguaji hao ni Mariam Sangwa,
Francine Bozi na Mary Sheli ambao tayari wameshatambulishwa kwenye maonyesho mbalimbali ya Akudo.
Meneja huyo alisema ujio wa wanenguaji hao unaifanya Akudo kuwa na jumla ya madansa sita wengine wakiwa ni Fanny Bosawa, Raissa Sangwa na Nadine Issala.
"Tumeongeza wanenguaji wakati huu ambao tuko kwenye maandalizi ya uzinduzi wa albamu
yetu ya History no Change ambayo itazinduliwa mwezi wa ujao," alisema Kyatika.
Alisema kuwa awali safu yao ya ushambuliaji wa jukwaa ilikuwa inapwaya hasa baada kupunguza baadhi ya wanenguaji ambao makali yao ya kufanya kazi yalikuwa yamepungua lakini sasa wamepata wapya.
Kyatika alizitaja baadhi ya nyimbo za albamu hiyo wanayojiandaa kuzindua kuwa ni 'Ubinafsi', 'Umefulia', 'Pongezi kwa Wanandoa' na 'Umejificha Wapi'.
Aliongeza kusema kuwa sasa Akudo imejipanga upya kuanzia kwenye uongozi wa bendi na
hivyo ana uhakika itaendelea kufanya vizuri kwa kuwaburudisha mashabiki na wapenzi wake.
Akudo imekuwa ikitamba na albamu yake ya kwanza ya Impact ambayo ilichangia kuipandisha chati bendi hiyo inayojiita Vijana wa Masauri ikiwa chini ya rais wake Christian Bella.

No comments:

Post a Comment