STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 3, 2011

Nyilawila awafunika Cheka, Maugo



BINGWA wa Dunia wa Ngumi za Kulipwa anayeshikilia taji la WBF, Karama Nyalawila, ndiye Mtanzania anayeongoza kwa ubora miongoni mwa mabondia wa uzani wa Middle akiwafunika wakali kama Francis Cheka na Mada Maugo.
Kwa mujibu wa takwimu za ubora wa mabondia wa uzani huo duniani, kupitia mtandao wa Box Rec, Nyalawila anashikilia nafasi ya 74, wakati Cheka, Bingwa wa Dunia wa UBO, ICB na WBC yupo nafasi ya 142.
Maugo yeye anashika nafasi ya 196 akimzidi wakongwe Rashid Matumla 'Snake Man' na Maneno Osward 'Mtambo wa Gongo' wanashika nafasi ya 327 na 370.
Nyalawila aliyetwaa taji hilo Desemba 3 mwaka jana huko Jamhuri ya Czech, ni miongoni mwa mabondia wanne wa kiafrika waliopo kwenye orodha wa mabondia 100 Bora Duniani wa uzani huo wa Middle.
Wengine waliopo kwenye orodha hiyo ni Mganda, Kassim Ouma anayeshika nafasi ya 32 akiwa ndiye kinara kwa mabondia wa Kiafrika, Assie Duran na Osumanu Adama wa Ghana waliopo nafasi ya 34 na 35 na Mnigeria, Eromosele Albert aliyepo anayeshikilia nafasi ya 38.
Bondia anayeongoza kwenye orodha ya wapiganaji wa uzani huo ni Sergio Gabriel Martinez wa Argentina anayefuatiwa na Felix Sturm wa Ujerumani na anmayeshikilia nafasi ya tatu duniani ni Danile Geale wa Australia.
Mabondia wa Kitanzania wanatengeneza 10 Bora yao wakiwafuata Nyalawila na Cheka ni, Mada Maugo (196), Thomas Mashali (212), George Dimoso (289), Maisha Samson (302), Rashid Matumla (327), Bagaza Mwambene (342), Stan Kessy (350) na Maneno Oswald 'Mtando wa Gongo' akiishika nafasi ya 370.

No comments:

Post a Comment