STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 3, 2011

Kanumba ana 'shock', Ray atamba





BAADA ya kuanza mwaka na filamu ya 'Deception', muigizaji nyota wa filamu nchini, Steven Kanumba 'The Great' ameibuka na filamu mpya iitwayo 'The Shock'.
Filamu hiyo ambayo imekamilika hivi karibuni na sasa ipo katika maandalizi ya kuachiwa mitaani, ni ya pili kwa msanii huyo kwa mwaka huu wa 2011.
Akizungumza na Micharazo, Kanumba alisema kama ulivyo utaratibu wake wa kuibua wasanii wapya katika fani hiyo, ndani ya 'The Shock' amemtambulisha muigizaji mpya mwanadada mrembo Shez Sadry ambaye amedai amefanya mambo makubwa kama mzoefu.
Kanumba alisema mbali na mwanadada huyo ambaye ndiye mhusika mkuu, pia kuna kuna muimbaji wa FM Academia Patcho Mwamba, Ben Braco, yeye mwenyewe na wengineo.
"Baada ya Deception sasa The Shock inakuja ambayo na kifaa kipya lakini kikali katika muigizaji, Shaz Sadry," alisema Kanumba.
Alisema filamu hiyo inatarajiwa kuachiwa mitaani ndani ya mwezi huu na itasambazwa na kampuni ya Steps Entertainment.
Katika hatua nyingine, mpinzani mkubwa wa Kanumba, Vincent Kigosi 'Ray' amesema filamu yake mpya ya 'Second Wife' inatarajiwa kuingia mitaani wiki ijayo na kuwataka mashabiki wa fani hiyo kukaa mkao wa kula kupata uhondo.
Katika filamu hiyo mpya, Ray ameigiza na wakali kama Riyama Ally, Coleta Raymond, Aisha Bui, muigizaji mpya mwanadada Skyner Ally na mtoto Aisha.
Ray amesema filamu hiyo ni 'funika bovu' kutokana na jinsi alivyoigiza kwa kushirikiana na wenzake na kusisitiza kuwa, hizo ni salamu kwa wapinzani wao kuwa RJ Production imekuja kivingine ndani ya mwaka 2011.

No comments:

Post a Comment