STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Thursday, March 3, 2011

Madee asikitika Dogo Janja kuzinguliwa shuleni

MSANII nyota wa muziki wa kizazi kipya, Hamad Ally 'Madee' amedai kusikitishwa na kitendo ambacho amekuwa akifanyiwa msanii chipukizi anayemfadhili, Abdul-Aziz Chende 'Dogo Janja' na mmoja wa walimu wa Shule ya Sekondari ya Makongo anayosoma kwa sasa.
Akizungumza na Micharazo, Madee alisema kuwa, amesikitishwa na taarifa kwamba mmoja wa walimu wa shule hiyo amekuwa akimpa wakati mgumu Dogo Janja, jambo analohofia linaweza kushuka kiwango chake cha elimu darasani.
Hata hivyo Madee alisema tayari suala la mwalimu huyo ambaye hakumtaja jina, limeshafikishwa kwa mkuu wa shule hiyo, na Dogo Janja anaendelea kusoma kwa vile hana mpango wa kuhama.
"Kwa walimu wa namna hii wanaharibu viwango vya wanafunzi darasani, ila nashukuru mambo yameshamalizwa kwa Dogo kwenda kwa Mkuu na kulalamika na ticha huyo kuonywa," alisema.
Aliongeza ni vema walimu wakatambua kuwa wao ni walezi kwa wanafunzi na hivyo waishi
kama watoto wao na wanapokosea wawaelekeze hata kama kwa bakora, lakini wakizingatia
miiko na taaluma zao za kazi.
Dogo Janja, alinukuliwa na kituo kimoja akisema kuwa alikung'utwa na mwalimu wake huyo baada ya kutofautiana nae kiswahili, huku akidai mara kwa mara amekuwa akimzingua akimuita 'Dogo Jinga' badala ya jina lake la Dogo Janja, kitu kilichokuwa kikimnyima raha shuleni.
Madee, aliamua kumsaidia Dogo Janja mwenyeji wa Arusha kutokanan na kuvutiwa na kipaji chake na tayari ameshamkamilishia albamu mpya iitwayo Ngarenaro, akiwa pia ndiye anayemlipia ada shuleni hapo akijiandaa kumfyatulia video ya albamu hiyo yenye nyimbo 10.

No comments:

Post a Comment