STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 26, 2011

Maugo kuzichapa na Mkenya



BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Mada Maugo anatarajiwa kupanda tena ulingoni jijini Mwanza kuzipiga na Mkenya, ikiwa anatokea kuuguza kipigo toka kwa Francis Cheka.
Aidha bondia huyo amesema hayupo tayari kupigana tena na Francis Cheka, labda kama mwamuzi na majaji watakuwa ni wa kutoka nje ya nchi kwa kile alichodia waamuzi na majaji wa nchini humbeba mpinzani wake kila mara.
kizungumza na MICHARAZO, Maugo, alisema pambano hilo la Mkenya Mosses Odhiambo litafanyika Novemba kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
Maugo, alisema pambano hilo lisilokuwa la ubingwa la raundi 10 na la uzani wa kati, ni maalum kwa maandalizi ya kwenda kupigana nje ya nchi katika pambano la kimataifa dhidi ya Mjerumani.
"Natarajia kupanda ulingoni mwezi Novemba kupigana na Mkenya katika pambano la raundi 10 la uzito wa kilo 72, lisilo la ubingwa kwa nia ya kujiweka fiti kabla ya kwenda kupigana ngumi za kimataifa dhidi ya Mjerumani," alisema Maugo.
Kuhusu kurudiana na Cheka, Maugo alisema atakuwa radhi kufanya hivyo kama majaji na waamuzi watatoka nje ya nchi kwa madai wa ndani humbeba mpinzani wake kama ilivyotokea kwenye mechi zao mbili ambapo zote alipigwa kwa pointi.
"Sintakuwa tayari kupigana tena na Cheka, labda kama waandaaji watawaleta majaji na mwamuzi kutoka nje, mpinzani wangu wamekuwa akibebwa ndio maana rekodi yake nje ya nchi ni mbovu tofauti na anavyotamba akicheza nyumbani," alisema.
Alisema wiki iliyopita akifuatwa na mmoja wa mapromota akiwataka wapigane na Cheka katika pambano la kusaka mbabe kati yao, na kuweka msimamo wake huo, hali iliyofanya muaandaji huyo kuamua kuachana na wazo la kuwapiganisha tena.
Maugo alipigwa kwa pointi na Cheka katika mapambano yaliyofanyika Januari Mosi, jijini Dar es Salaam na Septemba Mosi, mjini Morogoro, ambapo kote bondia huyo alikuwa akilalamikia 'kuchakachuliwa' matokeo.

No comments:

Post a Comment