STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Monday, September 26, 2011

Watanzania hawana utamaduni wa kusoma-EZAA





CHAMA cha Waandishi wa Vitabu Kanda ya Mashariki, EZAA, kimesema asilimia kubwa ya watanzania hawana utamaduni wa kupenda kusoma vitabu, jambo linalochangia kuwepo kwa ugumu wa soko la vitabu nchini.
Katibu Mkuu wa chama hicho, Jackson Kalindimya, aliyasema hayo wakati wa semina ya siku tatu ya watunzi wa vitabu vya hadithi za watoto, iliyofanyika kwenye ukumbi wa Msukuma, mjini Mlandizi, Pwani.
Kalindimya alisema Tanzania ina tatizo la watu kupenda kusoma, kitu ambacho kwa kiasi kikubwa kimekuwa kikiathiri soko la vitabu na maandishi mengi.
Hata hivyo, aliwaasa waandishi na watunzi wa vitabu kutokata tamaa badala yake kuzidi kuandaa kazi zenye mvuto ambavyo zitachochea wananchi kubadilika na kuanza kupenda kusoma kama ilivyo kwa mataifa mengi.
Kalindimya alisema tofauti na wananchi wa mataifa mengine ambao wawapo safarini au mahali popote hubeba vitabu au majarida kwa ajili ya kujisomea, kwa wananchi wa Tanzania ni wachache wanaofanya hivyo, kitu alichotaka watanzania wabadilike.
"Wananchi wanapaswa kubadilika na kujenga tabia ya kupenda kusoma kwani itawasaidia kuelimika, sambamba na kusaidia soko la kazi za waandishi," alisema.
"Licha ya hali hiyo, watunzi na waandishi msikate tamaa, muikabili changamoto hiyo kwa kuandaa kazi zenye mzuri zenye mvuto ambazo zitawabadilisha wananchi, pia ikirahisisha soko la kazi zenu," alisema.
Baadhi ya washiriki wa semina hiyo, ambao ni chipukizi katika utunzi na uandishi wa vitabu, waliwapongeza waandaaji wake kwa namna walivyowasaidia kuelewa mambo ambayo kabla ya hapo walikuwa hawana ufahamu nayo katika fani hiyo.

No comments:

Post a Comment