STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 18, 2011

Bondia Moro amtaka Miyeyusho

BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa mkoani Morogoro, Maneno William 'Chipolopolo' ameibuka na kudai anamtaka bingwa wa UBO-Mabara, Francis Miyeyusho wa Dar es Salaam, ili apigane nae.
Chipolopolo aliyejipatia umaarufu mkubwa mkoani humo, kutokana na uwezo wake wa kurusha makonde makali ulingoni, hivi sasa yuko katika mazoezi makali chini ya mwalimu Boma Kilangi.
Akizungumza na blog hii kutoka Morogoro, bondia huyo alisema amejipanga vizuri kufanya maajabu katika mchezo wa ngumi huku kiu yake kubwa ikiwa ni kuchapana na Miyeyusho maarufu kama 'Chichi Mawe'.
Chipolpolo, alisema anamuona Miyeyusho ni bondia wa kawaida na kwamba atapigika kirahisi licha ya kufanya vizuri katika mchezo huo katika siku za hivi karibuni.
Alisema, ili kutimiza dhamira yake yupo tayari kupanda ulingoni wakati wowote kuzipiga na Miyeyusho kama atatokea promota wa kuwaandalia pambano hilo.
Bondia huyo wa Morogoro alisema licha ya Miyeyusho kumchapa Mbwana Matumla hivi karibuni katika ukumbi wa Diamond Jubilee Dar es Salaam, ni lakini kwake lazima apate kipigo.
"Nipo fiti, najiamini na nafikiri sasa ni wakati wa kuchapana na Miyeyusho na kizuri zaidi ni bondia wa uzito wangu," alisema.
Chipolopolo alisema hachagui mahali pa kupambana na bondia huyo na kwamba yupo tayari kuvaana naye hata jijini Dar es Salaam.
MIcharazo lilijaribu kumsaka Miyeyusho kwa njia ya simu kupata maoni yake juu ya tambo za bondia huyo wa Morogoro, lakini hakuweza kupatikana.

Mwisho

No comments:

Post a Comment