STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Friday, November 18, 2011

Mabondia 10 kuwasindikiza Nassib vs Kariuki


BINGWA wa zamani wa Dunia wa World Boxing Forum, Juma Fundi na Rashid Ally ni miongoni mwa mabondia watakaolisindikiza pambano la kimataifa kati ya Nassib Ramadhan 'Manny Pacquiao wa Tz' dhidi ya Anthony Kariuki kutoka Kenya.
Nassib anayeshikilia kwa sasa taji la dunia la World Boxing Forum baada ya kumvua Juma Fundi Mei mwaka huu, atapigana na Karikuki katika pambano litaklofanyika siku ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru, Desemba 9 kwenye ukumbi wa DDC Keko, jijini Dar es Salaam.
Mratibu wa pambano hilo, Pius Agathon, aliiambia MICHARAZO kwamba Fundi na Ally ni kati ya mabondia 10 watakaopanda ulingoni kusikindikiza pambano hilo la raundi 10 lisilo la ubingwa kati ya Nassib na Kariuki.
Agathon, alisema Fundi atapigana siku hiyo na Juma Seleman katika pambano la raundi sita la uzani wa kilo 51, Fred Sayuni dhidi ya Bakar Dunda na Ramadhani Kumbele ataonyeshana kazi na Shabaan Madilu.
"Mipambano mingine siku hiyo itakuwa ni kati ya Rashid Ally atakayepigana na Daud Mhunzi katika uzito wa kilo 57 na Faraji Sayuni ataumizana na Alfa George ndipo Nassib atakapopanda ulingoni kupigana na Kariuki katika uzani wa Fly," alisema.
Mratibu huyo alisema maandalizi ya jumla ya mapambano hayo yanaendelea vema ikiwemo kumalizana na mabondia wote ambao kwa sasa wanaendelea kujifua kwa mazoezi tayari kuonyeshana ubabe siku hiyo kwenye ukumbi huo wa DDC Keko.
Aliongeza lengo la michezo hiyo mbali na kuwaweka fiti mabondia hususani Nassib ambaye mwakani atalitetea taji lake la World Boxing Forum, pia ni maalum kwa ajili ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru.
"Tumeandaa michezo hii ikiwa ni sehemu ya kuadhimisha miaka 50 ya Uhuru sambamba na kumuandaa vema Nassib kabla ya kulitetea taji lake mwakani," alisema.

Mwisho

No comments:

Post a Comment