STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 12, 2011

Maugo kuweka kambi Mwanza kumwinda Mjerumani



BONDIA machachari wa ngumi za kulipwa nchini, Mada Maugo anatarajia kuingia kambini jijini Mwanza, kujiandaa na pambano lake la kimataifa la kuwania ubingwa wa IBF dhidi ya Mjerumani Rico Nicovic atakayepigana nae Desemba 26 jijini humo.
Maugo ameiambia MICHARAZO kuwa, anatarajia kuondoka jijini Dar es Salaam wiki ijayo kwenda kuweka kambi jijini Mwanza tayari kumkabili mpinzani wake huyo katika pambano litakalofanyika kwenye uwanja wa CCM Kirumba.
Bondia huyo alisema kambi na pambano hilo la kimataifa litakalosimamiwa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa nchini, vyote vimeandaliwa na kugharamiwa na Mbunge wa Jimbo la Rorya, Lameck Airo 'Obama'.
"Maandalizi ya pambano langu yanaendelea vema nikiwa nimeshanza kuzungumza na mabondia watakaosindikiza siku hiyo na wiki ijayo natarajia kuondoka Dar kuelekea Mwanza kuweka kambi kwa ajili ya pigano hilo," alisema Maugo.
Aliongeza pambano lake na Mjerumani huyo, litakuwa la raundi 12 katika uzani wa kilo 72.5 na watasindikizwa na michezo zaidi ya mitano itakayowahusisha pia mabondia wakongwe nchini akiwemo bingwa wa zamani wa dunia wa WBU, Rashid Matumla.
Maugo alisema Matumla atapigana na bondia kutoka Uganda, huku Emma Kichere na mabondi wengine wa kanda ya Ziwa watapanda ulingoni kuonyeshana kazi sambamba na kuhamasisha mchezo katika kanda hiyo.
"Mkongwe Matumla atakuwepo kunisindikiza siku ya pambano langu na Nicovic, kuba analofanya mfadhili wangu, yaani Mbunge wa Rorya ni kuhamasisha ngumi katika kanda ya ziwa," alisema Mada.
Maugo, hivi karibuni alipata ushindi wa KO kwa kumpiga Joseph Odhiambo katika pambano lisilo la ubingwa ikiwa ni baada ya kutoka kupokea kipigo toka kwa Francis Cheka katika pambano la kuwania taji la UBO-Inter Continental.

Mwisho

No comments:

Post a Comment