STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 12, 2011

Jumbe, atambia Shoka la Bucha

UONGOZI wa bendi ya Talent umedai kuwa, albamu yao mpya inayoendelea kuandaliwa itakuwa moto kuliko ile ya kwanza ya 'Subiri Kidogo' ambayo inaendelea kubamba sokoni.
Mkurugenzi wa bendi hiyo, Husseni Jumbe, alisema maandalizi wanayofanya kuipika albamu yao ya pili itakayofahamika kama 'Shoka la Bucha' ni ya aina yake kitu kinachompa jeuri kwamba itafunika kuliko ile ya awali.
Jumbe, alisema tayari wamesharekodi nyimbo nne kati ya sita za albamu hiyo katika studio za Sound Crafters na mara watakapomaliza mbili za mwisho wataanza kurekodi video kabla ya kufanya uzinduzi na kuziingiza sokoni mapema mwakani.
"Nadhani Shoka la Bucha itafunika zaidi kuliko Subiri Kidogo kwa namna tunavyoiandaa kwa sasa tukiwa tumesharekodi nyimbo nne kati ya sita," alisema.
Jumbe, alisema tayari baadhi ya nyimbo hizo zilizorekodiwa zimeshasambazwa kwenye vituo vya redio ili kurushwa hewani.
Alizitaja nyimbo zilizorekodiwa hadi sasa ni Kilio cha Swahiba, Shoka la Bucha, Kiapo Mara Tatu na Jipu la Moyo.
Aliongeza, wapo kwenye mipango ya kufanyta ziara mikoani kwa nia ya kujitangaza zaidi sambamba na kuitambulisha albamu zao mbili, ikiwemo hiyo inayomaliziwa kurekodiwa.

No comments:

Post a Comment