STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 12, 2011

Young D, Aslay wote boda kwa boda




WASANII wanaokuja juu katika anga la muziki wa kizazi kipya nchini, Aslay Isiaka 'Dogo Aslay' na David Genz Mwanjela 'Young D' wanatarajia kuonyesha kazi watakapoungana na wakali wengine wa miondoko hiyo kwenye onyesho maalum litakalofanyika leo jijini Dar.
Dogo Aslay na Young D, wanaowatishia wakongwe wa muziki huo kwa namna ya kasi yao tangu walipoibuka, watashiriki tamasha lililopewa jina la 'Boda kwa Boda Beach Concert' ambalo litafanyikia kwenye ufukwe ya Mbalamwezi.
Mbali na wasanii hao wanaochuana kimuziki sambamba na chipukizi mwingine, Abdulaziz Chende 'Dogo Janja', pia tamasha hilo litawahusisha wakali kama msanii kutoka Kenya, Jaguar anayetamba na nyimbo za 'Kigeugeu' na 'Nimetoka Mbali' alioimba na nyota wa Tanzania, Ambwene Yesaya 'AY'.
Wengine watakaoshiriki tamasha hilo la 'Bodaboda' ni 'Mzee wa Hakunaga' Sumalee, Godzilla wa Salasala, Beca, Reycho, Country Boy & Stamina, na wengineo huku wakinakshiwa muziki huo na DJ Zero.
Kwa mujibu wa waratibu wa onyesho hilo, G5 Click, wakali hao watashirikiana pamoja kuangusha moja moja kuanzia saa moja jioni hadi 'kuchwee' ili kuwapa burudani mashabiki wa muziki wa kizazi kipya watakaoungana kwenye ufukwe huo.
"Ni tamasha la aina yake siku ya Jumamosi (leo) ambapo wasanii chipukizi na wakali wengine akiwemo Mkenya Jaguar watafanya vitu vyao katika ukumbi wa Mbalamwezi Beach Club."

No comments:

Post a Comment