STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 12, 2011

Coastal yawafuata Banka, Chuji Dar




UONGOZI wa klabu ya soka ya Coastal Union ya Tanga, imewafuata viungo nyota wa zamani wa Simba na Yanga, Mohammed Banka na Athuman Idd 'Chuji', ikipuuza taarifa kwamba Chuji ameamua kurejea Yanga kwa duru lijalo la Ligi Kuu Tanzania.
Mwenyekiti wa timu hiyo, Ahmed Aurora, alisema wanaamini Chuji ataichezea timu yao kama itakavyokuwa kwa Mohammed Banka na Ally Ahmed Shiboli ambao imekuwa ikiwanyemelea kukiimarish kikosi chao kwa duru hilo lijalo.
Aurora, alisema alikuwa akijiandaa kuja Dar ili kuonana na wachezaji hao watatu inayotaka kuwasajili kwenye dirisha dogo linalotarajiwa kufungwa Novemba 30.
"Klabu yetu bado inawahitaji wachezaji hao ili kuisaidia katika duru la pili na najiandaa kuja huko, licha ya kwamba nimeshtusha kusikia Chuji ametua Yanga, wakati tayari tulishaanza mazungumzo nae," alisema.
Aurora alisema hata kama Chuji atakuwa ametua Yanga (ingawa Yanga imemruka kimanga) bado wao watamfuata kuzungumza nae kabla ya kumsainisha mkataba wa kuicheza Coastal katika duru la Pili litakaloanza Januari mwakani.
Mbali na kuwawinda wachezaji hao, timu hiyo pia imetangaza kuwarudisha kundi nyota wake wa kimataifa, Mkenya Edwin Mukenya na Wanigeria wawili, Felix Amechi na Felix Amechi na Samuel Temi ambao walikuwa kwenye orodha ya usajili wa timu hiyo kabla ya kukwamba kutokana na sababu zilizokuwa nje ya uwezo wa pande mbili.
Coastal iliyorejea Ligi Kuu msimu huu ikitokea Daraja la Kwanza na timu nyingine tatu za Oljoro JKT, Moro United na Villa Squad, imemaliza duru la kwanza ikiwa katika nafasi tatu za kwanza toka mkiani baada ya kujikusanyia pointi 11 kwa michezo 13.

No comments:

Post a Comment