STRIKA

STRIKA

USILIKOSE

USILIKOSE

Saturday, November 12, 2011

BFT yapiga 'dochi' kozi ya makocha


KOZI ya ukocha wa ngumi ngazi ya kimataifa, iliyoandaliwa na Shirikisho la Ngumi za Ridhaa nchini, BFT ikishirikiana na Kamati ya Olimpiki Tanzania, TOC, imekwama kuanza leo Jumamosi kama ilivyopangwa badala yake sasa ifanyika Alhamisi ijayo.
Kozi hiyo itakayoshirikisha washiriki 30 watakaonolewa na Mkufunzi wa Kimataifa kutoka Algeria, ilikuwa imepangwa kuanza leo mjini Kibaha, lakini BFT imetoa taarifa kwamba imesogezwa mbele kutokana na kuchelewa kwa mkufunzi huyo.
Katibu Mkuu wa BFT, Makore Mashaga, alisema mkufunzi huyo, Azzedin Aggoune, aliwatumia taarifa za kupatwa na dharura na hivyo kutoweza kuwasili jana Ijumaa kama alivyokuwa amepanga ambapo sasa ameahidi kuwasili siku ya Jumatano..
Mashaga alisema kutoka na dharura hiyo iliyompata mkufunzi huyo wameona ni vema kuahirisha kozi hiyo na kutoa fursa kwa makocha walioteuliwa kushiriki kozi hiyo kushuhudia michuano ya ngumi ya Kova inayoendelea jijini Dar es Salaam.
"Ile kozi ya kimataifa ya ukocha wa ngumi iliyokuwa ianze Novemba 12-18 mjini Kibaha, imekwama kuanza kutokana na mkufunzi wa kimataifa toka Algeria kupatwa na dharura na kuchelewa kuja, sasa itaanza Novemba 17 huko huko Kibaha," alisema.
Mashaga alisema kozi hiyo inayotambuliwa na Shirikisho la Ngumi la Kimataifa, AIBA, itafungwa rasmi Novemba 25, ambapo washiriki watatunukiwa vyeti pamoja na wasifu wao kuwekwa kwenye database ya shirikisho hilo ili kuwaweza kutumika na kushiriki michuano yoyote ya kimataifa ya ngumi popote duniani.
Mmoja wa washiriki wa kozi hiyo, Rajab Mhamila 'Super D' alisema amefurahi kuteuliwa kushiriki kozi hiyo, akiamini itamsaidia kumpa ujuzi na kumjenga zaidi katika taaluma hiyo ya ukocha aayoifanya katika klabu za Ashanti na Amana zote za Ilala.

Mwisho

No comments:

Post a Comment